Habari njema kwa wakulima…
Kamati ya Taifa ya Mbegu (National Seed Committee) imeidhinisha matumizi ya aina 29 za mbegu mpya za mazao mbali mbali ya kilimo.
Mazao hayo ni mahindi, mpunga, alizeti, karanga na chai. Hatua hiyo ya Kamati inalenga kuongeza tija na kipato kwa mkulima.
Kuidhinishwa kwa aina hizo za mbegu kunafuatia mapendekezo yaliyofanywa na Kamati ya Taifa ya Kupitisha Aina Mpya za Mbegu za Mazao (The NationalVariety Release Committee) katika kikao chake kilichofanyika makao makuu ya Wizara ya Kilimo Mifugo na Uvuvi Dar-es-saalam tarehe 16 na 17 Machi 2016.
Jifunze zaidi kuhusu mbegu bora za mazao;
- Aina Bora 19 za Mbegu za Mihogo
- Jinsi ya Kuandaa na Kutunza Kitalu cha Mbegu ya Mpunga
- Zifahamu Mbegu Bora za Mahindi
Aina hizi mpya za mbegu zimepitishwa baada ya kufanyiwa utafiti na kugundulika kuwa zina sifa zifuatazo:
- Kutoa mavuno mengi
- Kustahimili ukame
- Ukinzani dhidi ya magonjwa na wadudu
- Kukomaa mapema na
- Kupendwa na wakulima.
Kati ya aina hizo mpya za mbegu, kuna aina 16 za mbegu za mahindi, 2 za mbegu za mpunga, 4 za mbegu za alizeti, mbegu za karanga 3 na 4 za mbegu za chai. Zipo pia mbegu 19 za mihogo.
Orodha ya aina mpya za mbegu za mazao
| TAASISI/KAMPUNI | ZAO | AINA YA MBEGU |
| Kituo cha Utafiti Seliani | Mahindi | SELIAN H215 |
| Kituo cha Utafiti Naliendele | Karanga | NARINUT 2013 |
| NACHI 2013 | ||
| KUCHELE 2013 | ||
| Kituo cha Utafiti Ilonga | Mahindi | WE4102 |
| WE4106 | ||
| WE4110 | ||
| WE4114 | ||
| WE4115 | ||
| Kituo cha Utafiti Tumbi | Mahindi | T104 |
| T105 | ||
| Kituo cha Utafiti Chollima Dakawa | Mpunga | CH-SAT01 |
| CH-SAT09 | ||
| Taasisi ya Utafiti wa Chai Tanzania | Chai | TRIT201/16 |
| TRIT201/43 | ||
| TRIT201/44 | ||
| TRIT201/55 | ||
| Sunflower Development Company (SDC) | Alizeti | NSFH36 |
| NSFH145 | ||
| Advanta Seed Company Ltd | Alizeti | AGUARA 4 |
| HYSUN 33 | ||
| Meru Agro-Tours & Consultancy Co. Ltd | Mahindi | MERU LISHE 503 |
| MERU LISHE 511 | ||
| IFFA Seed Co Ltd | Mahindi | KASPIDI HYBRID |
| KISONGO HYBRID | ||
| Krishna Seed Co Ltd | Mahindi | KRISHNA HYBRID-1 |
| KRISHNA HYBRID-2 | ||
| Aminata Quality Seeds & Consultancy Ltd | Mahindi | NATA H 401 |
| NATA K8 |
Mbegu hizo zimefanyiwa utafiti wa kina na vituo vya utafiti vya Umma na sekta binafsi hapa nchini. Sifa za aina hizo mpya za mbegu zilizoidhinishwa na Kamati ya Taifa ya Mbegu zimeambatanishwa hapa.
Aina hizo za mbegu zitaanza kuzalishwa na makampuni mbalimbali ya uzalishaji mbegu pamoja na Wakala wa Taifa wa Mbegu za Kilimo (Agricultural Seed Agency – ASA).
Lengo ni kuzifikisha aina hizo mpya za mbegu bora kwa wakulima kuanzia msimu wa 2017/2018.
Imetolewa na: Mh. Mwigulu Mchemba, Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi.

Naweza kupata walala wa mbegu ya DK 8031 kwa hapa Tanzania???
Nimeona maelekezo mbalimbali juu ya uzalishaji wa mazao ya mbogamboga na matunda je naweza kupata link ya kujua bei ya mazao hayo ya kila siku?
Tunashukuru
nimkulima wa dar es salaam, naomba kujua ubora wa mbegu ya muhogo aina ya kikombe
Mbegu za mihogo nitazipataje Mimi mkazi shinyanga
Mbegu zip ni bora kupanda ukanda wa magu
Swali la Ufahamu kuhusu kuadimika kwa Mbegu za Muda mfupi za DK 8031 katika mikoa ya Arusha na Manyara
Nahitaji mbegu mbora za mahindi na alizeti
Nipo igunga tabora
Mbegu bora ya mahindi ni ipi?
Nipate wapi namna ya kupambana na chumvi katika shamba la mpunga?
Mimi nataka kuanza kulima matikiti maji nipo pwani, naomba kujua mbegu zipi ni bora kulimia kupata mazao mengi kwa shamba la nusu Hekta pia naomba kujua mbegu punje moja inaweza kutoa matikiti maji mangapi. Ahsante
Mbegu vijijini hazipo zipo mjini NI changamoto kwa mkulima
Aina za mbegu zimekua nyingi natofauti unapoenda katika maduka ya pembejeo unaweza uziwa mbegu ambayo siobora tena kwagarama ukija upande wa mbolea inakua changamoto hili kama nyie wataalamu mmeliwekaje maana cy kila mtu atapata elimu