Matikiti maji hulimwa kama zao la biashara katika sehemu nyingi duniani zenye hali ya hewa ya joto la wastani. Zao hili lina wapatia watu shughuri za kufanya na hivyo kuwapatia kipato kuanzia kwenye nyanja za uzalishaji hadi kwenye matumizi. Matikiti maji ni mojawapo ya jamii aina ya matunda au mbogaboga inayotambaa. Mimea hii inapatikana katika kundi linalojumuisha mimea mingine (curcubitaceae family) kama matango, maboga na maskwash (squash).
Zao la tikiti maji ni mojawapo ya zao ambalo lina faida kubwa sana ukilinganisha na mazao mengine kwa muda mfupi. Katika shamba la ukubwa wa ekari moja (1 acre) lililoandaliwa vizuri, kupandwa na kuhudumiwa vizuri mkulima ana uwezo wa kuvuna kiasi cha tani 15-36, ambacho kitamsaidia kupata fedha za kukidhi mahitaji yake mbalimbali na kuondokana na umasikini.
Tikiti maji tayri kwa kuliwa
UCHAGUZI WA ENEO
Matikiti maji husitawi katika maeneo yenye joto la wasitani yaani haihimili hali ya joto kali sana, baridi kali, mvua nyingi wala udongo unaotuamisha maji, magonjwa ya fangasi na wadudu waharibifu.
Joto: Matikiti hukua vizuri katika maeneo yenye joto la wastani wa nyuzi kati ya 21 – 30 sentigradi. Iwapo mitikiti itapandwa katika maeneo yenye joto chini ya nyuzi 15 za sentigrade huchelewa kuota.
Mvua: Matikiti maji yanahitaji kiasi cha mvua kati ya millimita 400 – 600 kwa msimu. Mvua nyingi husababisha uwepo wa magonjwa ya fungasi na bakteria ambayo huathili mavuno.
Hali ya Udongo: Kilimo cha matikiti huhitaji udongo wenye rutuba nzuri ulio na virutubisho. Vile vile haihitaji udongo wenye kiasi kikubwa cha tindikali na alikali kubwa. Hali ya udongo katika kipimo cha pH iwe kati ya 6.0 na 7.0. Ingawa mmea una uwezo vile vile wa kuhimili kwenye udongo wenye pH 5.0
Mikoa ya Tanzania: Kilimo cha matikiti maji kinakubali vizuri kwenye ukanda wa pwani na miinuko kidogo kama DSM, Tanga, Morogoro, Mtwara, Lindi na Pwani ambapo kuna jua la kutosha. Muda mzuri wa kupanda ni kipindi cha kipupwe mwezi wa tatu mpaka wa tisa.
Fyeka vichaka na ng’oa visiki vyote. Katua kwa kina cha sm 22.5 kwenye Sesa. Kabla ya kupandikiza udongo utifuliwe vizuri na majani yaondolewe kabisa. Shamba liandaliwe vizuri kwa kusafisha ili kuondoa mimea mingine ambayo inaweza kuwa ni chanzo cha magonjwa. Weka mbolea ya samadi debe moja kwa kila mita 10 za eneo. Tengeneza matuta katika sehemu ambayo ina majimaji.
Upandaji wa tikiti maji
Katika shamba la ukubwa wa hekta moja kiasi cha kilo 3 – 4 cha mbegu kinaweza kutumika. Panda mbegu 2 au 3 moja kwa moja katika kila shimo. Usipande katika kitalu kwasababu miche ya mitikiti huwa ni dhaifu sana wakati wa upandikizwaji iwapo itapandwa kwenye kitalu hivyo kupelekea kufa kwa miche hiyo. Panda umbali wa sentimeta 2 chini ya udongo kwa umbali wa mita 1 hadi 2 kutoka shina hadi shina na mita 1.5 – 3 kutoka mstari hadi mstari.
Zingatia: usitumie mbegu za tikiti ulilonunua (kwa ajili ya kula) kwasababu linaweza kuwa ni chotara (Hybrid) ambayo hupelekea kushusha kiasi na ubora wa matikiti yatakayo zaliwa kwa sababu yatakuwa ni kizazi cha pili (F2).
Mbegu Bora za Matikiti
Mbegu maarufu ya tikiti ni Sukari F1, hata hivo madukani zinapatikana nyingi bora na tofauti tofauti kama vile:
Mimea ya mitikiti huanza kuota, baada ya kama wiki 2 hivi. Hivyo katika mbegu mbili au tatu ulizopanda kata moja na uache ile miche yenye afya zaidi ndio uendelee kukua. Ni vizuri ukaacha miche miwili katika kila shimo.
Angalizo: Usinga’oe mche bali ukate ili kuzuia kusumbua mizizi ya mche uliobaki. Vilevile unaweza kupandishia udongo kwenye mashina ili kusaidia kupunguza maji kutuama kwenye mimea yako, pia unaweza kuweka samadi badala ya kupandishia udongo ukiwa na nia ileile ya kuzuia maji yasituame na kuongeza rutuba. Kama una sehemu ndogo ya shamba unaweza kuyawekea matikiti waya wa kutambalia, ila inabidi uwe imara kwa sababu ya kuhimili uzito wa matunda. Wakati mimea inapo anza kutambaa kwenye waya ni lazima uifundishe (kuielekezea) kwenye waya na kuifungia.
Shamba linatakiwa limwagiliwe mara kwa mara wakati mvua zinapokosekana au wakati wa mvua chache. Kipindi muhimu zaidi ambapo mimea hii huhitaji maji ni katika kipindi cha uotaji wa mbegu, wakati wa kutoa maua na siku takribani kumi kabla ya kuvuna. Iwapo kutakuwa na ukosefu wa maji kutasababisha kutengenezwa kwa matunda ambayo si mazuri na yenye umbo baya, pia kupungua kwa ukubwa wa tunda.
Angalizo: usimwagilie matikiti wakati wa jioni sana au usiku kwasababu inaweza kusababisha magonjwa ya majani kutokana na unyevu kukaa muda mrefu. Vile vile usimwagilie juu ya maua wakati wa asubuhi au jioni kwasababu unaweza kuzuia wadudu kama nyuki ambao ni muhimu sana wakati wa uchavushaji.
Mbolea ya kupandia: Wakati wa kupanda tumia DAP weka gram 5 kwa kwa kila shimo (lenye mbegu moja, na weka gram 10 au 15 kama kuna mbegu 2 au 3), hakikisha mbolea na mbegu havigusani.
Mbolea ya kukuzia: Wiki mbili baada ya miche yako kuota weka mbolea ya kiwandani NPK (Yaramila winner) gram 5 tena kwa kila mche, hakikisha unaichimbia chini na isigusane na mmea. Weka mbolea yenye Calcium kama Yaramila nitrabo au CAN gram 10 kwa kila shina unapoona matunda yameanza ili kusaidia kupata matunda makubwa na mazuri.
Kwa ekali 1 ya matikiti utahitaji mfuko mmoja wa DAP, mmoja wa NPK na mmoja wa CAN ikiwa utabakiza miche miwili kwa kila shimo.
Hivi ukiwa shambani unawezaje kupima gram 5 au 10 za mbolea? Ni vigumu lakini kwa makadirio ya karibu ujazo wa kifuniko kimoja cha maji safi au soda take-away ni sawa na gram 5 hivyo ili upime gram 10 jaza vifuniko viwili vya maji safi. Soma hapa mahitaji ya mbolea katika mahindi
Matandazo (Mulches)
Matandazo ina maana ya kutumia nyasi na mabaki ya mimea mingine kufunika aridhi. Baada ya miche kutambaaa kwa kiasi unaweza kuweka matandazo (mulches) ambayo yaweza kuwa nyasi kavu kwenye udongo ili kuzuia upotevu wa unyevu vile vile kupunguza uotaji wa magugu shambani kwako. Vile vile matandazo yakioza yanaongeza rutuba kwenye udongo na hulinda udongo dhidi ya mmomonyoko wa udongo.
Matikiti maji shambani
WADUDU NA MAGONJWA YA TIKITI MAJI
Wadudu wa matikiti wako wa aina mbalimbali na wanaoshambulia sehemu za majani na maua, na wengine hushambulia matunda, pia kuna magonjwa ya fangasi ambayo hushambulia mimea.
Magonjwa kama ukungu wa unga (powdery mildew) na wa chini (Downy mildew) na mengine yathibitiwe kabla hayajaleta madhara kwenye mimea. Ili kujua dawa za magonjwa ni vizuri kuchukua sampuli na kwenda nayo kwenye duka la dawa na pembejeo za kilimo ili kupata dawa sahihi. Dawa aina ya Mancozeb inaweza kutumiwa kuthibiti magonjwa hayo hapo juu.
Vilevile matikiti hushambuliwa na wadudu ambao hukaa katika majani, maua na matunda. Dawa aina ya KARATE itasaidia kuua wadudu wa majani, maua na matunda. Soma hapa magonjwa ya nyanya na dawa zake
UVUNAJI NA UHIFADHI WA MATIKITI
Matikiti maji ni miongoni mwa mazao yanayochukua muda mfupi sana kukomaa. Kwa kawaida tikiki maji huwa tayari kwa kuvuna baada ya siku 80 hadi 100 baada ya kupanda. Vuna wakati tunda limeiva kabisa. Vuna kwa wakati unaofaa. Epuka kulijeruhi tunda. Hifadhi katika eneo lenye ubaridi nyuzi 15 hadi 20 C. Hifadhi vizuri, unyevua-anga (humidity) uwe 80 hadi 85%. Uza mara tu baada ya kuvuna shambani.
Ukipanda matikiti yako kwa nafasi ya 1m x 2m utakua na mashimo 2000 ya kupanda mbegu zako. Ikiwa kila shimo utapanda mbegu tatu na ukapunguzia mche mmoja na kuacha miwili ikue basi utakua na mimea 2 x 2000 = 4000.
kwa hiyo kwa ekali moja utakua na mimea 4000 ya matikiti. haya tufanye umeipunguzia matunda na hivyo kuufanya kila mmea uzae matunda mawili tu hivyo tunatarajia utavuna matunda 2 x 4000 = 8000.
Hivyo basi katika ekali moja ya matikiti uliyopanda kwa nafasi ya 1m x 2m ukakuza mimea 4000 utapata matunda 8000!
Tuchukulie mathalani umeamua kuuza matikiti yako shambani kwa bei ndogo kabisa ya Tsh. 1000 kwa tikiti moja, ukiuza matikiti yote 8000 utapata jumla ya Tsh. 1000 x 8000 = Tsh. 8,000,000 (Milioni nane)!
Inawezekana kabisa kuwa huu mchanganuo ni wa nadharia tu lakini ndugu yangu tumechukulia makadirio ya chini sana. Unajua ni kwanini?
Angalia hapa:
Mmea mmoja unaweza kuzaa matunda mangapi? We unajua lakini licha ya hayo yote sisi tumechukulia matunda mawili tu kwa mmea mmoja.
Pia bei ya tikiti inategemea ukubwa wake lakini sisi tumechukulia yote ni sawa na tunauza kwa bei moja tu.
Halafu pia bei ya matikiti tumechukulia ni Tsh 1000 tu wakati inaweza kuwa hadi Tsh 2000 uki-target wakati mzuri kwa soko.
Bila shaka utakuwa umenielewa vizuri sana, sasa fursa nimeiweka mikononi mwako na nimekufumbua macho yako, kazi kwako ndugu yangu. Lakini pia waweza kupitia namna ya kuzalisha matango na mananasi kisasa. Usisahau kuacha comment yako hapa chini.
I like blogging. In order utilize my profession I chose to share, to blog, a few tips and tricks about farming and agriculture to anyone interested.
57
Leave a Message
33Comment threads
24Thread replies
11Followers
Most reacted comment
Hottest comment thread
21Comment authors
Recent comment authors
Subscribe
newestoldestmost voted
Guest
Glory kamugisha
Asante kwa elimu nzuri ….ila kunauvumi unasema kuwa kuna mbegu na dawa feki za Tikiti maji sasa basi utajuaje kama hii ni mbegu /dawa halisi na sio feki ?
Njia nzuri ni kuangalia “lebo” ya uthibitisho kwenye paketi ya mbegu au kopo la dawa. Kwenye paketi ya mbegu bora kuwe na nembo ya TOSCI – hii ni taasisi rasmi ya kuthibitisha mbegu bora kabla ya kuuzwa kwa wakulima. Na makopo/paketi za dawa ziwe na nembo ya TPRI – taasisi rasmi ya utafiti wa viatilifu
Nakutakia mafanikio mema kaka Francis Deni, itakuwa vizuri ukitujuza unavyoendelea kwa faida ya wengi
Guest
Eliya
Habari, mimi nimejarib kulima matikiti huko kigambon lkn nilichokipata ni maumivu, nimelaza laki saba nimeambulia laki mbili na nusu. Nimeona hapa muda unaotakiwa lkn mwenyej wangu aliniambia ni miez miwili tu na nilipanda F1ya Kenya. Ila naomba kuuliza coz humu ndani sijakiona, Je ni kweli wiki moja ya mwisho unatakiwa usimwagie ili tunda liweke sukari? Naomba kuwasilisha
Pole sana kwa yaliyokufika. Mara baada ya matikiti kutoa matunda, yanapokuwa makubwa unatakiwa kupunguza maji kadri yanapoelekea kukomaa (refusha “irrigation interval”) kama ilikuwa mara mbili kwa wiki basi iwe mara moja kwa wiki au wiki mbili.
Pia ni muhimu matitiki yapate muda wa ukame kwa wiki au zaidi, kabla ya kuvuna, ili yaweke sukari nyingi zaidi.
nashukuru kwa elimu yako nzuri sana.nakuhakikishia nitaifanyia kazi fulsa hii na kwa mpango wa mungu nitafanikiwa na wewe ushukuriwe kwani naamini umenisogeza hatua moja mbele
Labda pia naombeni kuondolewa wasiwasi juu ya kilimo hiki.je jipi kuhusu mkoa wa kagera wilaya ya muleba kilimo hiki ni rafiki wa mazingira?Vipi kuhusu vipimo hivi vya pH,mm za mvua na kiwango cha jotoridi na ubaridi nitavipataje mimi mtu wa hali ya chini kikipato?mbegu na mbolea naweza kuzipata wapi kwa urahisi?vipi kuhusu bei ya vitu hivyo nilivyovitaja?nitashukuru nikipata majibu kupitia email yangu ya [email protected]
Mazingira / Hali ya hewa ya Muleba haina tatizo na kilimo cha matikiti maji.
Vitu kama mbegu na mbolea vinapatikana katika maduka ya pembejeo za kilimo ama kwa suala la bei: Urea kwa kawaida ni Tsh 50,000, CAN ni Tsh 55,000 na DAP ni 80,000. Hizo ni bei kulingana na mazingira ya kwetu, hata hivyo bei zinaweza kubadilika kulingana na mazingira kwa hiyo inaweza kupungua au kuongezeka kidogo kwa niliyotaja mimi.
Kuhusu vipimo vya Ph, joto na mm za mvua: hivi vinahitaji maelezo ya kutosha kwani ni changamoto kwa wakulima wengi. Hivyo nitaanza makala maalum kwa ajili hiyo.
kilimo cha matikiti katika ukanda wa mto ruvu (mlandizi) kinaweza kukubali bila kuathiri uzalishaji na ubora wa tikiti kama masharti yote ya kilimo hicho yakifwatwa? nikimaanisha hali ya hewa ya eneo inaruhusu?
Napimaje ardhi ili kujuwa rutuba kama ina fahaa kwa hicho kilimo cha matikiti..!!? je naweza ku chota udogo wa eneo la shamba nakwenda wanako uza pembejeo na mbegu za mimea wana weza kupima pia..? au sehemu stahiki ni ipi..ili nijirizishe na eneo stahiki..!!?
Lengo la kupima udongo laweza kuwa kujua pH ya udongo au kiwango cha virutubisho kwenye udongo wako. Na hii inafanywa na wataalam (kuandaa sampuli ya udongo shambani, na kisha) kupima sampuli kwenye maabara ya kupima udongo au kwa vifaa maalum vya kupimia.
Guest
Sebastian
kwa mikoa ya Kanda ya ziwa zao hili linaweza kukua vizuri? hasa mkoa wa kagera na geita
Habari, mimi naomba kuuliza maana nimeshalima matikiti nimekula hasara Ile mbaya, maswal yangu ni 2,.lnasemekana unaweza kulima matikiti mara nne kwa mwaka je unaweza kuniambia ni miez ipi? Swal la pili, wanasema kwamba matikiti yakishakomaa kipindi cha mwisho kama wiki mbili au moja na nusu unayakatia maji ili yaweke sukari, na hili likoje? Naomba kuwasilisha
Pole kwa yaliyokufika. Swali la kwanza: Ukitumia green house, unaweza bila shida. Lakini kwa shamba la wazi ni lazima uepuke maji ya mvua wakati wa maua, lkn pia uhakikishe hakuna maji ya kutuama na mwisho ujidhatiti kudhibiti wadudu na magonjwa ya fungus.
Kwa swali la pili: Jibu ni ndio. Ili kuongeza sukari, matitiki yanahitaji kipindi fulani cha ukame usio na madhara. Kukata maji wiki au mbili kabla ya kuvuna kunaweza kufaa.
Guest
Nick
Vijana wajiunge vikundi then wajichange hata kidogo waanze na eneo dogo nguvu zao zitumike kuhudumia shamba, baada ya mavuno mtaji Utaongeza ndipo waweze kuchukua eneo kubwa
Nitatizo gani husababisha tikiti maji kuwa na uwazi unapolibonyeza na wakati mwingine kupasuka sehemu ya nyuma/kwenye kitovu chake
Guest
Magero komesi
Mie humu ni mgeni ninahitaji kujifunza kuhusu kilimo na ufugaji
Guest
Bernard manota
Kwa majina yangu naitwa MR.BERNARD MANOTA Mr.mtalula Mohammed Kwa upande wangu niseme asante saana kwa elimu yako , niseme2 kuwa mie nakupenda saana hikibkilimo cha matiki maji hapo niliwahi kulima na nikaambulia hasala lakini kuna mambo ambayo niliyabaini kutokana na kutokuwa na uzoefu, kwa sasa nimejipanga kuwekeza tena katika Kilimo hiki , nikiwa lini n kuongea na bwana mmoja akanishauli kutumia mbengu sina ya “JULIANA” Naomba kuuliza Je Juliana na baby sukal Na African Queen Kati ya hizi mbegu IPI ilivyo bora saaana kushinda zote hapo? Pia nilikuwa nahitaji kupata kitabu cha mwongozo wa Kilimo hiki ,,,,na Kilimo cha vitunguu,,,,,,… Read more »
Guest
Kingu
Nataka mtu anayetokea maeneo wanakolima tikiti my no 0758507208
Guest
0784280573
Nashukuru kwa maelezo mazuri nahitaji kujua zaia na kupata vitabu zaidi
Guest
Johnson winfred
Asanta kwa elimu…nimelima tikiki kuanzia mwezi wa sita kati kati kuna baadhi ya miche imesha toa matunda bt miche mingine ndo kwanza imetoa mauwa hivi sasa bcz nilipata changamoto ya maji kipindi cha upandaji. Je haita nipa shida katika kipindi cha kuvuna??
Karoti ni zao la jamii ya mzizi. Karoti ni aina ya mboga mboga yenye vyanzo vingi vya calcium, iron na wingi wa vitamin B. kilimo cha karoti huhitaji ...
Tatizo la nyanya kuoza kitako ni hali ya kifiziolojia inayosababishwa na uchache wa au mmea kushindwa kufyonza madini ya chokaa (Calcium) kwenye udongo ...
Ni muhimu kujua jinsi ya kuandaa na kutunza kitalu cha miche ya mbogamboga kwa sababu mazao mengi ya mboga mboga huhitaji kuanzia kitaluni ili yaweze ku...
Asante kwa elimu nzuri ….ila kunauvumi unasema kuwa kuna mbegu na dawa feki za Tikiti maji sasa basi utajuaje kama hii ni mbegu /dawa halisi na sio feki ?
Njia nzuri ni kuangalia “lebo” ya uthibitisho kwenye paketi ya mbegu au kopo la dawa. Kwenye paketi ya mbegu bora kuwe na nembo ya TOSCI – hii ni taasisi rasmi ya kuthibitisha mbegu bora kabla ya kuuzwa kwa wakulima. Na makopo/paketi za dawa ziwe na nembo ya TPRI – taasisi rasmi ya utafiti wa viatilifu
Enter your comment…number yangu jamanii 0753389875 nahitajii uo ufundi wa matikiti
Nimejipanga ili kuhakikisha natumia elimu niliyoipata humu ndani na kuifanyia kazi
Nakutakia mafanikio mema kaka Francis Deni, itakuwa vizuri ukitujuza unavyoendelea kwa faida ya wengi
Habari, mimi nimejarib kulima matikiti huko kigambon lkn nilichokipata ni maumivu, nimelaza laki saba nimeambulia laki mbili na nusu. Nimeona hapa muda unaotakiwa lkn mwenyej wangu aliniambia ni miez miwili tu na nilipanda F1ya Kenya. Ila naomba kuuliza coz humu ndani sijakiona, Je ni kweli wiki moja ya mwisho unatakiwa usimwagie ili tunda liweke sukari? Naomba kuwasilisha
Pole sana kwa yaliyokufika. Mara baada ya matikiti kutoa matunda, yanapokuwa makubwa unatakiwa kupunguza maji kadri yanapoelekea kukomaa (refusha “irrigation interval”) kama ilikuwa mara mbili kwa wiki basi iwe mara moja kwa wiki au wiki mbili.
Pia ni muhimu matitiki yapate muda wa ukame kwa wiki au zaidi, kabla ya kuvuna, ili yaweke sukari nyingi zaidi.
Nimependezwa sana na elimu ya kilimo cha matikiti maji.Ntalifanyia kazi na ntaletà mrejesho hapa
Karibu sana
Nimepanda bila Sukari F1 tarehe 5.10.2019 ila sijapanda kwa mbolea yeyote ni mbolea gani inafaa kwa kukuziaa.
Thanx kwa somo zuri
Shukrani, karibu sana
Mambo ni mazuri sana endelea kutuelimisha
kikubwa ni mtaji tu,kweli kilimo kinalipa
kikubwa ni mtaji tu,kweli kilimo kinalipa
Karibu sana, Endelea kuwa nasi
nashukuru kwa elimu yako nzuri sana.nakuhakikishia nitaifanyia kazi fulsa hii na kwa mpango wa mungu nitafanikiwa na wewe ushukuriwe kwani naamini umenisogeza hatua moja mbele
Ahsante sana, fanya juhudi M/Mungu atakuwezesha. Usisahau ku-subscribe kwa mengi mazuri yajayo
Labda pia naombeni kuondolewa wasiwasi juu ya kilimo hiki.je jipi kuhusu mkoa wa kagera wilaya ya muleba kilimo hiki ni rafiki wa mazingira?Vipi kuhusu vipimo hivi vya pH,mm za mvua na kiwango cha jotoridi na ubaridi nitavipataje mimi mtu wa hali ya chini kikipato?mbegu na mbolea naweza kuzipata wapi kwa urahisi?vipi kuhusu bei ya vitu hivyo nilivyovitaja?nitashukuru nikipata majibu kupitia email yangu ya [email protected]
Mazingira / Hali ya hewa ya Muleba haina tatizo na kilimo cha matikiti maji.
Vitu kama mbegu na mbolea vinapatikana katika maduka ya pembejeo za kilimo ama kwa suala la bei: Urea kwa kawaida ni Tsh 50,000, CAN ni Tsh 55,000 na DAP ni 80,000. Hizo ni bei kulingana na mazingira ya kwetu, hata hivyo bei zinaweza kubadilika kulingana na mazingira kwa hiyo inaweza kupungua au kuongezeka kidogo kwa niliyotaja mimi.
Kuhusu vipimo vya Ph, joto na mm za mvua: hivi vinahitaji maelezo ya kutosha kwani ni changamoto kwa wakulima wengi. Hivyo nitaanza makala maalum kwa ajili hiyo.
Habari!!
Asante kwa elimu hii ya tikiti maji!!
kilimo cha matikiti katika ukanda wa mto ruvu (mlandizi) kinaweza kukubali bila kuathiri uzalishaji na ubora wa tikiti kama masharti yote ya kilimo hicho yakifwatwa? nikimaanisha hali ya hewa ya eneo inaruhusu?
Asante!!!!
Ndio, Kinakubali
Nitumie pdf ya Kilimo cha matikiti, nimesha lipia 1000 kwenye Airtel money
Habari naomba namba yako ili tuweze kuwasiliana ili uweze kunielekeza 1kama kuna kulipia Huduma you n.a.
2 ili niweze kupata maelekezo zaidi
Namba yangu ni +255 655 570 084
Asante sana kwa elim zur VP mkoa Wa Ruvuma matikiti yanaweza kustaw
Ndio, yanastawi
Nimefaidika sana na elimu ya kilimocha tikiti maji……
Karibu sana
Nimejipanga kupiga pesa tu
Nashukuru kwa somo hili. Naomba number yako tafadhali
Wadudu hujawataja
Kwenye maboresho yajayo tutaweka!
+255 655 570 084
Napimaje ardhi ili kujuwa rutuba kama ina fahaa kwa hicho kilimo cha matikiti..!!? je naweza ku chota udogo wa eneo la shamba nakwenda wanako uza pembejeo na mbegu za mimea wana weza kupima pia..? au sehemu stahiki ni ipi..ili nijirizishe na eneo stahiki..!!?
Lengo la kupima udongo laweza kuwa kujua pH ya udongo au kiwango cha virutubisho kwenye udongo wako. Na hii inafanywa na wataalam (kuandaa sampuli ya udongo shambani, na kisha) kupima sampuli kwenye maabara ya kupima udongo au kwa vifaa maalum vya kupimia.
kwa mikoa ya Kanda ya ziwa zao hili linaweza kukua vizuri? hasa mkoa wa kagera na geita
Naam! Linaweza kumea vizuri tu
Habari, mimi naomba kuuliza maana nimeshalima matikiti nimekula hasara Ile mbaya, maswal yangu ni 2,.lnasemekana unaweza kulima matikiti mara nne kwa mwaka je unaweza kuniambia ni miez ipi? Swal la pili, wanasema kwamba matikiti yakishakomaa kipindi cha mwisho kama wiki mbili au moja na nusu unayakatia maji ili yaweke sukari, na hili likoje? Naomba kuwasilisha
Pole kwa yaliyokufika.
Swali la kwanza: Ukitumia green house, unaweza bila shida. Lakini kwa shamba la wazi ni lazima uepuke maji ya mvua wakati wa maua, lkn pia uhakikishe hakuna maji ya kutuama na mwisho ujidhatiti kudhibiti wadudu na magonjwa ya fungus.
Kwa swali la pili: Jibu ni ndio. Ili kuongeza sukari, matitiki yanahitaji kipindi fulani cha ukame usio na madhara. Kukata maji wiki au mbili kabla ya kuvuna kunaweza kufaa.
Vijana wajiunge vikundi then wajichange hata kidogo waanze na eneo dogo nguvu zao zitumike kuhudumia shamba, baada ya mavuno mtaji Utaongeza ndipo waweze kuchukua eneo kubwa
Ushauri mzuri kwa vijana wenye nia ya dhati. Shukran
Keep it up br, najua utasaidia watanzania wengi kwa elimu hii ya bure. Mungu akusaidie pia
Amin. Shukran sana kwa kunitia moyo
Najihusisha na Kilimo
IKO VIZURI
Nitatizo gani husababisha tikiti maji kuwa na uwazi unapolibonyeza na wakati mwingine kupasuka sehemu ya nyuma/kwenye kitovu chake
Mie humu ni mgeni ninahitaji kujifunza kuhusu kilimo na ufugaji
Kwa majina yangu naitwa MR.BERNARD MANOTA Mr.mtalula Mohammed Kwa upande wangu niseme asante saana kwa elimu yako , niseme2 kuwa mie nakupenda saana hikibkilimo cha matiki maji hapo niliwahi kulima na nikaambulia hasala lakini kuna mambo ambayo niliyabaini kutokana na kutokuwa na uzoefu, kwa sasa nimejipanga kuwekeza tena katika Kilimo hiki , nikiwa lini n kuongea na bwana mmoja akanishauli kutumia mbengu sina ya “JULIANA” Naomba kuuliza Je Juliana na baby sukal Na African Queen Kati ya hizi mbegu IPI ilivyo bora saaana kushinda zote hapo? Pia nilikuwa nahitaji kupata kitabu cha mwongozo wa Kilimo hiki ,,,,na Kilimo cha vitunguu,,,,,,… Read more »
Nataka mtu anayetokea maeneo wanakolima tikiti my no 0758507208
Nashukuru kwa maelezo mazuri nahitaji kujua zaia na kupata vitabu zaidi
Asanta kwa elimu…nimelima tikiki kuanzia mwezi wa sita kati kati kuna baadhi ya miche imesha toa matunda bt miche mingine ndo kwanza imetoa mauwa hivi sasa bcz nilipata changamoto ya maji kipindi cha upandaji. Je haita nipa shida katika kipindi cha kuvuna??
Hapana Johnson haiwezi kukupa shida. Matikiti huyavunwi yote kwa mara moja, yanavunwa kwa awamu kulingana na kukomaa kwake.
Thanks in advance the materia are well organised.
Habari asante kwa taarifa nzuri, naomba kufahamu zaidi kuhusu kilimo hiki hasa upande wa masoko ya uhakika
Gwakisa kutokea Mbeya-Tanzania
Asante sana Mr. Mtalula masomo yako yananisaidia katika kazi zangu
Nimewapenda kwa maelekezo yenu asanteni sana