Kilimo cha Viazi mviringo na Faida zake kwa Wakulima Tanzania
Viazi mviringo ni miongoni mwa mazao makuu kumi ya chakula nchini Tanzania, na ni zao la tatu baada ya mahindi na mpunga kiuzalishaji. Kiasi kikubwa cha viazi mviringo kinazalishwa katika ukanda wa nyanda za juu kusini unaojumuisha mikoa ya; Njombe, Mbeya, Songwe na Iringa.
