Unapoanzisha mradi wa kilimo biashara, unatarajia mwisho wa siku uumalize kwa kupata faida, sasa basi leo nataka nikufahamishe mambo makubwa mawili unayotakiwa kuyajua kabla hujaanza mradi wako wowote wa kilimo.
Habari ndugu msomaji wangu, na pole kwa shughuri mbalimbali za ujenzi wa Taifa. Wiki iliyopita nilikuandikia makala inayokufahamisha Kilimo bora cha zao la muhogo lakini leo nimekuletea kitu cha tofauti kidogo. Unapoanzisha mradi unatarajia mwisho wa siku uumalize kwa kupata faida, sasa basi leo nataka nikufahamishe mambo makubwa mawili unayotakiwa kuyajua kabla hujaanza mradi wako wowote wa kilimo.
Jambo la kwanza: Hatua kwa hatua za utunzaji wa zao (Farming master-plan)
Katika kilimo biashara, hili ni jambo la kwanza na muhimu sana kulifahamu. Farming master-plan ni muongozo wa shughuri zote unazotakiwa kuzifanya katika kilimo chako tangu kuandaa shamba mpaka kuvuna.
Hii ijumuishe shughuri kama kupanda, kudhibiti magugu, uwekaji wa mbolea na kupulizia madawa ya wadudu na magonjwa. Unatakiwa kujua shughuri hizi zote, muda wa kuzifanya, namna ya kuzifanya na mahitaji yake ili uzifanye.
Kwa mfano uwekaji wa mbolea: wakati gani uweke? kiasi gani? uwekeje? Unatakiwa ufahamu haya yote kabla hujaanza mradi wako wa kilimo ilii usipate usumbufu wakati wa utekelezaji.
Jambo la pili: Makadirio ya Gharama za Uzalishaji na faida
Hili ni jambo lingine muhimu sana. Naamini unapofanya kilimo biashara hujaamua kulima ili ujifurahishe tu, unalima ili upate faida. Hivyo basi unatakiwa ujue mradi wako utakugharimu kiasi gani katika utekelezaji wake na mwisho wa siku utakulipa kiasi gani? Pengine hutopata gharama halisi lakini ni lazima ufahamuu japo makadirio ya gharama ili kwanza uweze kujipanga lakini pia usikwame katika utekelezaji wa mradi wako.
Kwanini ni muhimu kufahamu mambo haya?
- Utajua mahitaji muhimu unayotakiwa kuwa nayo kabla hujauanza mradi wa kilimo
- Utapata fursa ya kuuona mradi wako katika hatua mbalimbali hata kabla hujauanzisha
- Utaweza kujua makadirio ya gharama za uzalishaji na faida tarajiwa
Kwa hiyo nikunasihi ndugu yangu usianzishe mradi wako wa kilimo mpaka ujiridhishe kuwa una ufahamu wa mambo haya mawili.
Mogriculture Tz katika kuhakisha kuwa tunakurahisishia kilimo biashara, tunakuandalia miongozo miwili inayogusa vilivyo mambo hayo mawili kwa kila zao. Miongozo yenyewe ni Farming master-plan (Muongozo wa shughuri za tunzaji wa zao) na Production cost and benefit analysis (Mchanganuo wa gharama za uzalishaji na faida). Haya yote tumeyaweka kwenye kitabu kimoja ambacho tunakiita Mwongozo wa kilimo bora.
Gharama ya kila Mwongozo wa kilimo bora kwa kila zao ni TZS 10,000 tu. Kila mwongozo una gharama za uzalishaji na hatua zote muhimu za utunzaji wa zao mpaka kuvuna. Mpaka sasa miongozo iliyopo tayari ni kwa mazao ya Mahindi, Maharage, Matango, mpunga na vitunguu maji. Na mingine bado tunaifanyia kazi. Unaweza kuwasiliana nasi hapa.
Hiki ndicho nilichokuandalia kwa leo na natumai utakuwa umefaidika nacho. Kabla hujamaliza, nimekuchagulia baadhi ya makala ambazo nimeona zisikupite;
- Mambo yakufanya ili mkulima upate faida zaidi katika kilimo
- Kilimo cha kisasa cha bamia
- Kilimo bora cha karanga
Katika kilimo biashara, je kuna jambo lingine mkulima anapaswa kulifahamu na sijaeleza hapa? Tujuze kwenye comments.


Nawashukuru Sana ktk mchango wenu wa uendelezaji wa kilimo chenye tija kwa Mkulima.ningependa kujua nimikoa ipi iliyokwisha kupimwa na wataalam kwa kuzalisha kilimo cha muhogo?
Soma hapa: https://www.mogriculture.com/muongozo-wa-kilimo-cha-muhogo/
ahdanteni sana kiukweli nimejifunza sana mazuri leo kutokana na makala haya
Endelea kuwa nasi kwa mengi mazuri
Mwanza wilaya za sengerema na geita pia inakubali san
Kazi nzuri mno,Ahsanteni sana.
Ahsante, endelea kuwa nasi
Asante sana kwa maarifa yaliyo bora sana.
Rafiki yako,
Aliko Musa.
Kazi Yenu ni njema sana.
Nimejifunza na nitaendelea kuwafatilia ,nimeona mna vitu vizuri sana.
Je gunia la mahalage Kuna kilo ngapi?
kwa kawaida ni kg 120